Kiungo Wa Manchester United Paul
Pogba Amejiunga Na Timu Yake Hiyo Kwenye Mazoezi Katika Uwanja Wa Carrington
Mapema Hapo Jana Kujiandaa Na Mchezo Wa Ligi Ya England Dhidi Ya Chelsea
Utakaopigwa Siku Ya Jumapili Ya November 5 Katika Dimba La Stanford Bridge.
Paul Pogba Akiwasili Katika Uwanja wa Mazoezi wa Manchester United Carrington.
Pogba ‘24’ Alipata Majeraha Kwenye
Mchezo Dhidi Ya Fc Basel Klabu Bingwa Ulaya Na Kushindwa Kuitumikia Timu Yake
Kwenye Michizo 11 , Lakini Kiungo Huyo Anatarajiwa Kurejea Kisosini Wikiend Hii
Baada Ya Kuanza Mazoezi Na Wachezaji Wenzake.
Mchezo Wa Hapo Kesho United Itawakosa Fellaini, Michael Carrick, Zlatan Ibrahimovic Na Marcos Rojo Ambao Bado Wanauguza Majeraha Yao Na Kocha Jose Mourinho Amesema Anapata Wakati Mgumu Kutokana Na Majeruhi Lakini Anaamini Wachezaji Wake Watapata Matokeo Japo Kuwa Mchezo Huo Utakuwa Mgumu.
Kuelekea Mchezo wa Kesho Chelsea na Manchester United wanaingia katika mchezo wa Jumapili katika kupunguza pengo la pointi dhidi ya Vinara wa ligi Manchester City , Kocha Jose Mourinho Anarudi Katika Dimba lake la Nyumbani la Zamani Baada Kujiunga na United katika kipindi cha kiangazi cha mwaka 2016 Akitokea Chelsea .
Amekuwa na
Rekodi ya Kushinda mechi 5 kati ya 9 dhidi ya vilabu alivyowahi kuvifundisha
katika maisha yake ya ukocha, amefungwa mechi 3 na sare 1.Ushindi
wa 1-0 dhidi ya Benfica ugenini ulimaliza mfululizo wa kupoteza mechi za
ugenini dhidi ya vilabu vyake vya zamani.
Chelsea
wanaingia katika mchezo wa Jumamosi wakiwa wana rekodi ya kupoteza mechi 1 tu kati
ya 15 walizocheza vs United katika uwanja wa Stamford Bridge. Wameshinda 9 na
kutoa sare 5. Msimu uliopita walimtandika Mourinho 4-0 darajani.
Chelsea – Bakayoko mwenye majeruhi ya groin, David Luiz
(paja), Hazard (achilles), Kanté (hamstring), Morata (match fitnes) – wana hati
hati ya kucheza.




No comments:
Post a Comment